• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Hanang DIstrict Council
Hanang DIstrict Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Hanang

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mpango Mikakati
  • Utawala
    • Organization Structure
    • Idara
      • Utawala na utumishi
      • Fedha na Biashara
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ufugaji na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii na Ustawi
      • Ujenzi
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Uchaguzi
      • Ugavi na Manunuzi
      • Mali Asili
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
    • Viwanda
    • Biashara
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma kwa Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Whe. Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Madiwani
      • Kamati ya Fedha,Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maji
      • Kamati ya Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Ukimwi
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • On coming Project
    • On going Projects
    • Completed Projects
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za shughuli za ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

KAMATI YA FEDHA HANANG’ YARIDHISHWA NA MAENDELEO YA MIRADI, YAIPONGEZA HALMASHAURI,

Posted on: April 24th, 2025

Kamati ya Fedha, Uongozi na Mipango ya Halmashauri ya Wilaya ya Hanang’ leo imefanya ziara ya kukagua utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo inayotekelezwa katika kipindi cha robo ya tatu ya mwaka wa fedha 2024/2025, inayoishia mwezi Machi 2025.

Ziara hiyo imeongozwa na Mwenyekiti wa Halmashauri hiyo, Mhe. Rose Kamili, na ililenga kufuatilia kwa karibu utekelezaji wa miradi ya kimkakati inayogusa moja kwa moja maisha ya wananchi.

Katika hatua ya awali ya ziara hiyo, Kamati ilitembelea Shule ya Msingi Bomani, ambako inaendelea ujenzi wa shimo la choo kwa ajili ya wanafunzi, mradi unaolenga kuboresha mazingira ya usafi na afya shuleni, hasa katika kipindi hiki ambacho usafi wa mazingira ni kigezo muhimu cha maendeleo ya elimu bora.

Baada ya hapo, wajumbe wa kamati walielekea Shule ya Msingi Katesh B ambako walikagua ujenzi wa vyumba vya madarasa pamoja na matundu kumi ya vyoo. Mradi huu umeelezwa kuwa ni sehemu ya jitihada za kupunguza msongamano wa wanafunzi darasani na kuboresha hali ya kujifunzia kwa watoto.

Kamati hiyo ilieleza kuridhishwa na kasi ya ujenzi na usimamizi wake, na kutoa wito kwa jamii kuendelea kushirikiana na serikali kuhakikisha miradi inakamilika kwa wakati.

Akizungumza wakati wa ukaguzi wa mradi mwingine mkubwa wa ujenzi wa stendi ya kisasa ya mabasi ya Dkt. Samia, Mhe. Kamili alisema kuwa stendi hiyo ni kielelezo cha dhamira ya Halmashauri katika kuboresha huduma za usafiri na kuinua uchumi wa wakazi wa Hanang’ na maeneo ya jirani. Stendi hiyo inatarajiwa kuwa kitovu muhimu cha biashara, ajira na usafirishaji katika Wilaya hiyo.

Wajumbe wa kamati walisifu hatua iliyofikiwa katika ujenzi wa stendi hiyo, wakisema kuwa maendeleo yaliyopo yanaonesha jinsi ambavyo Halmashauri kupitia Mkurugenzi Mtendaji wake imejizatiti kusimamia utekelezaji wa miradi kwa ufanisi.


Aidha, walimpongeza Mkurugenzi kwa kufuatilia kwa karibu hatua zote za utekelezaji na kuonesha uongozi makini unaolenga kuleta matokeo chanya kwa wananchi.

Kwa ujumla, ziara hiyo ya Kamati ya Fedha, Uongozi na Mipango imeonesha kuwa miradi ya maendeleo katika Wilaya ya Hanang’ inaendelea kutekelezwa kwa ufanisi mkubwa, huku usimamizi wa karibu kutoka kwa viongozi wa Halmashauri ukitajwa kuwa moja ya sababu za mafanikio hayo.

Kamati imeahidi kuendelea kufuatilia utekelezaji wa miradi mingine ili kuhakikisha rasilimali za umma zinatumika kwa manufaa ya wananchi.



Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI - HANANG DC October 22, 2024
  • FOMU ZA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA SHULE ZA SEKONDARI WILAYA YA HANANG 2023 December 03, 2022
  • MATOKEO YA USAILI KWA KADA YA MTENDAJI WA KIJIJI III NA KADA YA DREVA II September 12, 2022
  • TANGAZO LA KUKODISHA SHAMBA LA GAWAL NA BASSOTU August 18, 2022
  • View All

Latest News

  • JENGO LA WODI YA WAZAZI HOSPITALI YA TUMAINI MBIONI KUKAMILIKA , LATOA MATUMAINI MAPYA KWA WAKAZI WA HANANG’

    May 14, 2025
  • UBORESHAJI WA DAFTARI LA WAPIGA KURA: WAANDISHI WASAIDIZI NA WAENDESHA VIFAA VYA BAYOMETRIKI WAPEWA MAFUNZO HANANG.

    May 14, 2025
  • CCM YARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI HANANG’

    May 13, 2025
  • MADIWANI WAPONGEZA UONGOZI KWA HALMASHAURI KWA USIMAMIZI BORA WA MIRADI YA MAENDELEO

    May 07, 2025
  • View All

Video

Mh. Rais John Pombe Maghufuli akitoa onyo juu ya vyombo vya habari
More Videos

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu za Leseni za Biashara

Viunganishi Linganifu

  • Watumishi Portal
  • Tovuti yaUtumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali ya Tanzania
  • Tovuti ya Mkoa wa Manyara
  • Tovuti TAMISEMI
  • Mamlaka ya Vitambulisho Tanzania (NIDA)

Watembeleaji wa Kimataifa

world map hits counter

Idadi ya Watembelea Tovuti

free HitCounter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Hanang' District Council Headquater located at the Northern part of Katesh town in Ganana Ward

    Postal Address: P.O Box 02 Katesh-Hanang'

    Telephone: 027-2530022 / 42

    Mobile: +255 762 362 950

    Email: ded@hanangdc.go.tz

Mawasiliano yetu

   

    • Privacy Policy
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.